Nawezaje kudhibiti ugonjwa wa kisukari

From Audiopedia
Revision as of 17:22, 18 July 2023 by Marcelheyne (talk | contribs) (XML import)
(diff) ← Older revision | Latest revision (diff) | Newer revision → (diff)
Jump to: navigation, search

Ikiwa unaugua Aina 2 ya ugonjwa wa kisukari, muone mhudumu wa afya ili aweze kuchunguza viwango vya sukari kwenye damu yako, kuona ikiwa unahitaji dawa. Unaweza kudhibiti ugonjwa wa kisukari kwa kula vyema.

  • kula vyakula vidogo kila mara. Hii husaidia kudhibiti viwango vya sukari kwenye damu.
  • Usile vyakula vitamu kwa wingi.
  • Epuka vyakula vilivyo na mafuta mengi kama vile siagi, mafuta ya ng'ombe, mafuta ya nguruwe, isipokuwa tu kama unapata shida ya kupata chakula.
  • Kuna mimea ambayo inasaidia sana katika kudhibiti ugonjwa wa kisukari katika maeneo yake. Muulize mhudumu wako wa afya.

Ikiwezekana, hakikisha kuwa unamuona mhudumu wako wa afya kila mara kuhakikisha kuwa ugonjwa haujafika kiwango kibaya.

Ili kuzuia maambukizi na majeraha kwenye ngozi, sugua meno baada ya kula, oga na uvae viatu kuepuka majeraha miguuni. Kagua mikono na miguu yako mara moja kwa siku kuona ikiwa una vidonda. Ikiwa una kidonda na kuna ishara ya maambukizi (ni nyekundu, kimefura au kina joto) muone mhudumu wa afya.

Ikiwezekana, weka miguu juu unapopumzika. Hii inasaidia sana hasa ikiwa miguu yako inapoteza rangi na kuwa nyeusi au kufa ganzi. Hii ni ishara kuwa damu haitembei sawa sawa kwenye miguu miguu yako.

Sources
  • Burns, A. A., Niemann, S., Lovich, R., Maxwell, J., & Shapiro, K. (2014). Where women have no doctor: A health guide for women. Hesperian Foundation.
  • Audiopedia ID: sw010422