Ninapaswa kujua nini kuhusu ujauzito na uzazi
From Audiopedia
Kila mwanamke mjamzito anahitaji afya njema, chakula kizuri, upendo na msaada wa familia na jamii yake. Wanawake wengi huhisi sana afya nzuri wakati wa ujauzito na huwa bila shida yoyote wakati wa kujifungua. Watoto wengi huzaliwa wakiwa na afya njema.
Wakati uo huo, mimba inaweza kuhatarisha maisha ya mwanamke. Karibu nusu milioni ya wanawake hufariki kila mwaka kutokana na matatizo ya ujauzito na kuzaa (hii pia inaitwa vifo vitokanavyo na uzazi), haswa katika nchi maskini.
Vifo hivi vinaweza kuzuiwa na huduma za msingi. Sura hii ina habari ambazo zinaweza kusaidia wanawake wajawazito kujitunza wenyewe, au kusaidia wengine kuwatunza.