Ninawezaje kuzuia kichefuchefu

From Audiopedia
Jump to: navigation, search

Ingawaje huitwa 'ugonjwa wa asubuhi', unaweza kuhisi kutapika wakati wa uja uzito wakati fulani wa siku au hata siku nzima. Hisia hii hupotea mwisho wa mwezi wa 3 au wa 4.

Namna ya kuzuia kichefuchefu:

  • Kunywa kikombe cha tangawizi au mdalasini mara 2 au 3 kwa siku, kabla ya kula.
  • Kula viwango vidogo vidogo vya chakula, na usile vyakula vyenye mafuta mengi au vigumu kusaga.
  • Lamba ndimu.
  • Waulize wakunga katika jamii yako, dawa za kienyeji ambazo zinaweza kukusaidia.
  • Jaribu kula biskuti, kipande cha mkate, chapati, mchele au uji unapoamka asubuhi.

TAHADHARI: Muone mhudumu wa afya ikiwa unatapika kila unapokula, au kama unapoteza uzani. Angalia ishara za upungufu wa maji mwilini kama vile: kiu, kukosa haja ndogo, mdomo uliokauka, kuhisi kizunguzungu unaposimama, ngozi kukauka. Ikiwa una ishara hizi, na pia unatapika, unahitaji kupewa maji kwa sindano yaani IV. Tafuta huduma ya kimatibabu haraka iwezekanavyo. Kupungua kwa maji mwilini ni hali ya dharura.



Sources
  • Burns, A. A., Niemann, S., Lovich, R., Maxwell, J., & Shapiro, K. (2014). Where women have no doctor: A health guide for women. Hesperian Foundation.
  • Audiopedia ID: sw010708