Nafanya kazi mbali na nyumbani - je niendelee tu kumnyonyesha mtoto wangu
Wanawake wengi siku hizi hufanya kazi mbali na nyumbani. Hii inaweza kufanya mambo kuwa magumu kwa mama kumnyonyesha mtoto wake bila kumpa chakula kingine chochote katika miezi sita ya kwanza. Lakini mtoto wako aweza kuugua iwapo hapati maziwa yako. Mama anayefanya kazi hafai kamwe kujipata katika hali inayomhitaji kuamua kati ya kazi yake na afya ya mtoto wake.
Ndiposa akina mama wanaofanya kazi wanahitaji usaidizi. Kazi zingine zinawaruhusu akina mama kuwaleta watoto wao maeneo ya kazi kwa miezi kadha. Hii inafanya shughuli ya kunyonyesha mtoto kuwa rahisi. Iwapo mama ana mtunzi karibu naye, anaweza kumnyonyesha mtoto mchana, wakati wa mapumziko. Baadhi ya waajiri hujenga vituo vya kutunza watoto wachanga ili wazazi wawe karibu na watoto wao.
Hizi ni baadhi ya mbinu za kuhakikisha mtoto wako anapata tu maziwa ya mama wakati unafanya kazi:
MUHIMU: Maziwa ambayo hayawezi kuhifadhiwa katika mazingira baridi yataharibika na yanafaa kumwagwa yote. Iwapo maziwa yatakuwa na harufu chachu, yamwagwe. Maziwa ya mama yaliyoharibika yanaweza kumdhuru kabisa mtoto.